St. Augustine University of Tanzania-Songea

St. Augustine University of Tanzania-Songea
Creating a peaceful society

Thursday, May 21, 2015

Ardhi ya Tanzania inavyowanyonga Watanzania

Na Wanafunzi Mwaka wa Pili, 2015

HAKUNA ubishi kwamba ardhi ni kitu pekee katika dunia hii ambacho ni cha thamani kufanyia kazi, cha thamani kugombania kwalo, cha thamani hata mtu  kufa kwa ajii yake, kwasababu ndiyo kitu pekee ambacho kipo daima. Hii ni tafsiri ya Gerald O’Hara katika riwaya ya toweka na upepo (Gone with the wind).

Migogoro ya ardhi Tanzania ni chimbuko la uhasama kati ya wafugaji na wakulima, wafugaji, wakulima na serikali yao kunakosababishwa na kutokuwepo kwa mipaka, uwekezaji, kuuzwa na kuuziana kwa viwanja au mashamba ambapo chanzo kikuu cha migogoro hii ni ukosefu wa  elimu ya sheria ya ardhi kwa watanzania walio wengi.

Fursa inayoonekana kuwaneemesha waerevu wachache serikalini na miongoni mwa wananchi ambapo ujinga wao wakutojua sheria za ardhi inakuwa ni mtaji kwa werevu.

 Sheria ya Ardhi ya vijiji Na. 5 ya mwaka 1999 ni moja ya sheria ambayo  mikakati yake ni kutekeleza Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995. Sheria hizi zinaainisha vyombo pekee vya kushughulikia migogoro ya ardhi na nyumba ni Baraza la Ardhi la kijiji, Baraza la kata,  Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya, Mahakama Kuu – kitengo cha Ardhi na Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Lakini je, ni kwa kiasi gani wananchi wanatambua sheria hiyo? kama kunagharama je, wananchi wote wanaweza kumudu kufungua kesi au mashauri ya migogoro ya ardhi na hata pengine kuweka wakili? Je, mwananchi wa kawaida katika mazingira haya anaweza kupata haki yake kiurahisi endapo atapambana na werevu wanaoonekana wanamiliki fedha? Mimi sina majibu.

Ebu tuangalie mfano hai wa mgogoro huu wa viwanja kwenye kata ya Mshangano katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea.

Pascal Msigwa ni mfanyabiashara maarufu mjini Songea ambaye anaeleza kwamba eneo linalodaiwa kuwa ni la shule ya sekondari si kweli bali ni lake.

“mimi ninalaumiwa bure lakini kiukweli eneo linalotajwa kuwa ni eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa sekondari ni mali yangu halali kwa kuwa niliuziwa na afisa mmoja wa Idara ya ardhi Halmashauri ya Manispaa ya Songea.”Alisema Pascal Msigwa.

Alisema eneo hilo linalodaiwa kuwa lilitengwa kwaajili ya ujenzi wa sekondari Mshangano ni uzushi na ndiyo maana baada ya kutekeleza taratibu zote za kisheria za ardhi alipewa eneo hilo.
Kwa upande wake Mkurugezi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Zakaria Nachoo, alipoulizwa alikana kuhusika katika uuzwaji  wa kiwanja hicho na wala kujua kwamba kuna afisa wake alihusika kutoa eneo hilo kwa Msigwa.

Ingawa alisema anaufahamu mgogoro huo ambao kwa hivi sasa upo katika ngazi ya baraza la kata ambako bado tatizo hilo  linashughulikiwa ili kupatiwa ufumbuzi.

Nachoo alisema elimu kwa wananchi kuhusiana na sheria ya ardhi ni tatizo kubwa kwasababu katika mitaa mingi unakuta kwamba pamoja na kuwa viwanja vimepimwa lakini bado wananchi wanakuwa wakiingia katika migogoro aidha wenyewe kwa wenyewe ama kati ya wananchi na kampuni ya upimaji.

Akitolea mfano alisema kwasababu katika mitaa mingi unakuta kwamba pamoja na kuwa viwanja vimepimwa lakini bado wananchi wanakuwa wakiingia katika migogoro aidha wenyewe kwa wenyewe ama kati ya wananchi na kampuni ya upimaji.

Alifafanua kwamba mara nyingi wananchi katika mitaa husika wamekuwa katika migogoro hiyo kutokana na baadhi ya wenzao kuuza maeneo yasiyowahusu.

Utakuta mtu mwingine amepakana na mwenzake na yeye anataka kuuza eneo lake, matokeo kwa kuwa mteja pengine anataka eneo kubwa na kwa fedha nyingi basi mwananchi anauza na eneo ambalo si lake na kisha kupotea, huo ni ufafanuzi ambao aliutoa Mkurugenzi.

Alisema katika mazingira haya yameleta mitafaruku mingi kwenye Halmashauri yake ambapo watu wachache wanatengeneza maisha kutokana na werevu wao huku wakijuwa kwamba wananchi walio wengi hawana elimu.

Kata ya mshangano viwanja vyote vilipimwa na kampuni binafsi ijulikanayo kwa jina la “ARDHI PLAN LIMITED” inayomilikiwa na Samandito Gombo ambaye ni mkurugenzi wa kampuni.

Nachoo alieleza kwamba kabla ya upimaji maeneo hayo ya Mshangano wananchi walielezwa madhara ya upimwaji wa viwanja kwa utaratibu wa kampuni hiyo lakini hawakukubali.

Leo migogoro inaibuka wanakimbilia ofisini kwake kwa lengo la kuyapatia ufumbuzi jambo ambalo wananchi hao wangekubaliana na ushauri wao kabla sidhani kama migogoro hiyo ingefikia hatua iliyopo sasa.

Anaeleza katika moja ya tukio lililotokea mshangano hivi karibuni, mwananchi alipimiwa kiwanja na kwa mujibu wa mkataba wa kampuni hiyo ya upimaji wa aridhi, ilikuwa  kwa kila mtu mwenye kiwanja kimoja ama viwili gharama yake ni laki moja kwa kiwanja na laki mbili kwa viwanja viwili.
Kuanzia viwanja vitatu ilitumika sheria ya uwiano wa 60% kwa 40% ambapo mwanachi angebakiwa na viwanja sawa na asilimia 60% na kampuni kuchukua asilimia 40% kama malipo ya upimaji wa viwanja hivyo.

Kwa upande wake afisa Mtendaji wa mtaa wa Mshangano bwana Damas Mbele amesema kuwa bado wananchi wanafika ofisini hapo wakiwa na malalamiko kuhusiana na viwanja vyao.

Anaeleza kwamba jambo hili wanashindwa kulielewa kwa kuwa suala la upimwaji wa viwanja hivyo lilifanyika kwa maelewano na mikataba ya kisheria kati wananchi hao na kampuni husika sasa inakuwaje leo wanadai kitu walichotowa kwa hiari yao? Alihoji mtendaji.

“Inatokea mwananchi anakuja ofisini akidai kuwa kiwanja ama viwanja  ambavyo kampuni  imechukua  sivyo  ambavyo yeye alitaka kuipa kampuni na hivyo kufanya migogoro kuendelea kuwa mingi, kwa kweli jambo hili linatushangaza sana.” Alifafanua Mbele.

Anaeleza kwamba walipojaribu kufuatilia kwa undani wamegundua kuwa wananchi wameanza kudai tena viwanja vyao baada ya kuona kwamba wamemaliza fedha ambazo walizipata awali.

Hivyo wanaamini kuwa kama wataanzisha mgogoro huo basi watapata tena viwanja hivyo kwani kuna baadhi ya watu wanajifanya mabushi loya ambao wanawachochea wananchi hao ili wadai tena viwanja.

Huku lengo halisi la mabushi loya hao ni kutaka kujipatia fedha kutoka kwa wateja wengine kama endapo maeneo yatapatikana na kuuzwa tena kwa wateja wengine ambao wanakuwa tayari wamewaandaa.

Alieleza kwamba jambo lingine ambalo wananchi linawatesa sana ni pale wanapoona afisa ardhi anauza maeneo ambayo wakati wa kupimwa yalipimwa kwa majina ya watu tofauti lakini kuuza anauza mtu mmoja.

Alieleza tatizo hili ni moja ya chanzo cha migogoro kwani hata Halmashauri yao ya Manispaa ya Songea inachangia kwani hilo jambo la baadhi ya maafisa na madiwani kujigawia maeneo ni la muda mrefu lakini hakuna suluhisho la kudumu linalochukuliwa.


Pia mbali na hivo lakini kuna kesi pia za watu kuuza kiwanja kimoja mara mbili ambayo yote pia ni kutokana na  ukosefu wa elimu ya sheria ya ardhi na nyumba miongoni mwa wananchi wa Tanzania.  


No comments:

Post a Comment